Fahamu haya machache juu ya matokeo ya AJUCO
TATABLOG na mytatablog ilizungumza na wanafunzi Wa chuo hicho wamesema wanakishukuru chuo kujitahidi kiwezavyo pamoja na majukumu mengi ya uongozi wao wamefanikisha kutoa matokeo ,japo kunaonekana kuwepo na changamoto kadhaa katika utoaji Wa matokeo yao ikiwemo chuo bado hakijaweza kuandaa tovuti maalumu kwaajili ya matokeo kwani yanapo bandikwa yanatupa wakati mgumu kuangalia matokeo hayo ,alisema mwanafunzi huo
Mwingine alielekeza hoja zake kwenye ubandikaji Wa matokeo hayo na kusema kuwa, japo wametumia mbinu hii ya ubandikaji Wa matokeo sio mbaya ila kutokana na wingi tulionao sisi wanafunzi Wa mwaka Wa kwanza wangeweza kuyabandika katika sehemu mbili tofauti ili kuwezesha kila mmja kuyaona kwa urahisi wanapoyaweka sehemu moja yanaweza kuchanika ndani ya dakika chache na wengine wasiyaone kabisa alizungumza
Kwanini uongozi unabandika usiku matokeo na wengine kushindwa kuyaona kwa wakati kutokana na kuishi mbali na eneo la chuo .hivyo basi tunaomba uongozi katika matokeo yajayo wafanikishe zoezi la kuandaa tovuti ya matokeo kama vyuo vingine
Pia kumeonekana kuwepo na sintofahamu juu ya uchakataji Wa matokeo hayo kwani inaonekana mtu ana tamrini kubwa 30 na hata zaidi lakini jumla yake amepata D inamaana kuwa mtihani Wa mwisho kati ya 60 ana alama chache sana ambazo zimemfanya kushindwa kufikisha wastani unaohitajika na chuo alisema kijana mmja
mfano UDSM .ahsante. Ni maoni na ambayo nimeyapokea kama yalivyo
Comments